Katka ulimwengu wa teknolojia ya 5G Oppo wamekuwa wakijitahidi kutoa simu janja ambazo zina mashiko kutokana na kwendana na kile ambacho soko linataka. Simu janja Oppo Reno6 5G ni miongoni mwa rununu ambazo zinavutia.
Nimekuwa mfuatiliaji mzuri tuu wa simu janja ambazo zinatoka zikiwa na 5G na Oppo wamekuwa waking’ara kwenye mauzo kutokana na rununu wanazotoa. Katika pitapita zangu za huku na kule nikakutana na Oppo Reno6 5G ambayo imetoka na wenzake wengine wamili, uchambuzi wake utakuja hapo baadae lakini tuifahamu hii kwanza. Sifa zake ni kama ifuatavyo:-
Kioo :
- Ukubwa: Urefu wa inchi 6.43
- Ubora: AMOLED (1080*2400px, 90Hz); ina ung’avu wa hali ya juu sana kufanya kinachoonekana kivutie
Memori :
- Diski uhifadhi: 128GB/256GB
- RAM: GB 8 na 12
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 64, 8 na 2+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 32+uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4300 mAh
- USB-C 3.1, OTG+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 65W, inatumia “Super VOOC 2.0” ambayo inafanya chaji kujaa haraka
Kipuri mama :
- MediaTek Dimensity 900 5G
Uzito :
- Gramu 182
Programu Endeshi
- ColorOS 11.3, Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi, Zambarau na Bluu
- Bei yake inaanzia $424 (zaidi ya Tsh. 975,200) kwa bei ya ughaibuni
Rununu hii tayari imeshaingia sokoni ila kwa nchi zetu hatuna budi kuagiza au kama si lazima sana ni vyema tukasubiri mpaka hapo zitakapoanza kuonekana kwenye nchi tulizopo.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.