Kampuni ya Tecno inasifika kwa kutoa simu zenye thamani nzuri kwa pesa ya mnunuaji, zikiwa na faida kubwa kama kukaa na chaji kwa muda mrefu wa matumizi na pia kamera zenye ubora mzuri kwa matumizi mbalimbali ya upigaji picha. Simu hii ya Tecno Camon 15 inaendelea kuwa katika sifa hiyo ya thamani nzuri.
Simu hii hupatikana kwa takribani shilingi laki nne za kitanzania. Kiasi hiki huweza kuongezeka au kupungua kutegemeana na mahali pa ununuzi.
Sifa za Tecno Camon 15.
- Kioo (Display) cha teknolojia ya LCD chenye ukubwa wa inch 6.6
- Mfumo Endeshi wa Android 10.
- Chipset ya Mediatek Helio P22
- RAM ya GB 4 na diski uhifadhi yenye ukubwa wa GB 64
- Mfumo wa kamera nne nyuma (MP 48, 2, 2 na QVGA) na kamera ya MP 16 mbele
- Betri yenye uwezo wa 5000 mAh
Simu hii ina teknolojia ya utambuzi wa alama za vidole (Fingerprint). Pia, ina teknolojia ya mawasiliano ya 4G kwa ajili ya mtandao wenye kasi na pia ina teknolojia za WiFi na Bluetooth kwa ajili ya kuhirikisha data na taarifa nyingine. Pia, ina huduma ya FM Radio.
Simu hii ina sehemu ya kuchomeka waya wa chaji aina ya microUSB 2.0 na sehemu ya kuchomeka waya wa earphones. Ina matoleo matatu ya rangi, Dhahabu (Shoal Gold), Zambarau (Fascinating Purple) na Kijani (Jade).
No Comment! Be the first one.