Kampuni ya Oppo ni kampuni toka nchini Uchina inayokuja kwa namna nzuri katika nyanja ya simu janja duniani.
Simu hii ya Oppo A31 ni moja kati ya matoleo yao ya kiwnago cha kati yenye thamani nzuri na ujazo wa sifa mbalimbali zenye kufanikisha matumizi mazuri ya simu.
Baadhi ya sifa hizo ni:
- Kioo (Display) cha teknolojia ya LCD chenye ukubwa wa inch 6.5,
- MfumoEndeshi (OS) wa Android 9,
- Chipset ya Mediatek Helio P35,
- 64GB 4GB RAM, 128GB 4GB RAM, 128GB 6GB RAM,
- Mfumo wa kamera tatu nyuma (MP 12, 2 na 2) na kamera ya MP 8 mbele,
- Betri yenye uwezo wa 4230 mAh.
Simu hii ina teknolojia ya utambuzi wa alama za vidole (Fingerprint). Pia, inasapoti teknolojia ya mawasiliano ya 4G kwa ajili ya mtandao wenye kasi. Simu hii ina teknolojia za WiFi na Bluetooth bila kusahau huduma ya FM Radio.
Simu hii pia ina sehemu ya kuchomeka waya wa chaji aina ya microUSB 2.0, pia ikiwa na sehemu ya kuchomeka waya ya earphones. Matoleo ya rangi kwa simu hii ni matatu, Nyeupe, Nyeusi na Kijani.
Kiujumla bei yake inahimilika inayoanzia $355|zaidi Tsh. 816,500 kwa bei ya ughaibuni lakini pia rununu hii ipo sokoni kwa muda mrefu tangu itoke.
Vyanzo: GSMArena, Gadgets 360
No Comment! Be the first one.