Ubisoft ni moja kati ya kampuni kubwa sana inayojihusisha na maswala ya magemu, taarifa waliyoitoa ni kwamba wataacha kutoa huduma (ya kimtandao) kwa baadhi ya magemu yake maarufu
Huduma ambazo zinasitishwa ni pamoja na zile huduma za mtandaoni (online) na baadhi ya wachezaje watapoteza DLC zao
DLC (downloadable content) hizi ni baadhi ya vitu ambavyo unaweza nunua mtandaoni na kuviongezea katika gemu husika ili kurahisisha uchezaji n.k
Mfano unaweza nunua maisha, nguo, silaha .n.k… Kwa maana nyingine ni kwamba wachezaji watashindwa cheza kwa pamoja (multiplayer) sababu huduma hii inahitaji mtandao.
Kama kuna mahusiano yoyote ya kimtandao na muingiliano wa akaunti huko hautafanya kazi tena, vivyo hivyo wachezaji wana hati hati kbwa sana ya kupeteza kabisa DLC ambazo walizinunua
Magemu hayo ni
- Anno 2070
- Assassin’s Creed 2
- Assassin’s Creed 3
- Assassin’s Creed Brotherhood
- Assassin’s Creed Liberation HD
- Assassin’s Creed Revelations
- Driver San Francisco
- Far Cry 3
- Ghost Recon Future Soldier
- Prince of Persia: The Forgotten Sands
- Rayman Legends
- Silent Hunter 5
- Space Junkies
- Splinter Cell: Blacklist
- ZombiU
Kama ni mtumiaji wa vifaa vya PC, PlayStation 3, Wii U, na Xbox 360 hili linakuhusu kabisa mana hutaweza tena pata huduma ya magemu haya kama mwanzo.
Ningependa kusikia kutoka kwako, naindikie hapo chini katika eneo la comment, je hii umeipokeaje? Je unadhani ni wazo zuri kwa kampuni kafanya kitu kama hiki
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
One Comment