Kama kawaida lawama nyingi huwa zinawafikia maderva tuu ambao wanaendesha magari kwa kutumia Uber. Vipi kuhusu wateja wao sasa? ni mara chache sana utapata kusikia kuwa wateja hao wameshitakiwa.
Kazi kubwa inabakiaga tuu kwa madereva wa Uber ambapo huwa wanaadhibiwa na kampuni na hata wateja mufa mwingine katika sanduku la maoni huwa wanawatolea sifa mbaya (wanazostahili baada ya kukiuka makubalino/sheria) au hata kuto wapa nyota zao.
Kwa madereva kupata maoni ya kusifiwa na kuwa na nyota za kutosha ni kitu cha msingi sana kwao kwani tangia mara ya kwanza wanavyojiunga na mtandao huo huwa wanaambiwaga.
Kwa mfano dereva ambae ana nyota chache sana na katika eneo lake la kuachia maoni lina malalamiko mengi kuhusu yeye basi Uber wenyewe wanaweza kuchukua jukumu la kumuondoa kabisa katika mtandao huo.
Hii itakua ni hivyo hivyo hata kwa wasafiri ambao wanatumia Uber, ni wazi kabisa kuwa Uber wanaweza mfuta msafiri katika App yao baada ya yeye kwenda kinyume na taratibu pangwa.