Twitter imekuwa ni miongoni mwa mitandao ya kijamii ambayo inafanyiwa maboresho ya mara kwa mara kutokana na sababu mbalimbali kitu ambacho kinaifanya kuwa ya kitofauti. Je, unafahamu kuhusu uwezo wa kutoa angalizo kuhusu chapisho?
Mtandao wa kijamii wa Twitter si kivutio kibwa cha vijana wengi duniani lakini ukiwa mtumiaji wa mara kwa mara basi utaona raha ya kuwa akaunti huko. Mwaka jana, Twitter iliweka wazi kuhusu kuleta kipengele ambacho kinamuwezesha yule anayetaka kupandisha chapisho kutoa angalizo kuhusu kile anachotaka kuonyesha wanaomfuata.
Kipengele hiki hakipo kwenye majaribio tena na tayari kimeshapelekwa kwenye watumiaji wa Twiter upande wa iOS, Android na hata kompyuta ambapo mhusika anaweza kutoa angalizo kwamba chapisho husika lina maudhui fulani (picha/video ya kutisha, watu walijeruhiwa/kufa, n.k).
Wakati wa kupandisha chapisho iwapo chapisho hilo lina maudhui fulani basi utabonyeza kitufe cha “Edit” kisha kubofya alama ya kibendela ambacho ndani yake kuna menyu ndogo itatokea na kuweza kuchagua iwapo kitu hicho kinaonyesha picha/vidoe za utupu, ugomvi au vitu ambavyo havitakiwi kuonwa na wengi.
Hatua hii inasaidia kuondoa taharuki kwa wale wanakufuatilia kwenye mtandao wa Twitter kwani kabla ya kufungua chapisho husika linakuwa halionkani vizuri na lina ujumbe wa kutahadharisha kuwa hiki kinachoonekana hapo ndani yake kina maudhui ya aina fulani.
Haya sasa watumiaji wa Twitter ule wakati wa kushangaa kutokana na chapisho uliloliona umekwisha kwani tahadhari inatoka hata kabla hujafungua kuona kilichomo.
Vyanzo: The Verge, Mashable
No Comment! Be the first one.