Mtandao wa kijamii wa Twitter wakanusha vikali habari ya kwamba wana uwezo wa kusoma nywila (passwords) za watumiaji wa mtandao wao wa Vine, mtandao wa kijamii unaohusisha utumaji wa video fupi.
Kwa mujibu wa OurMine(kundi linalojishughulisha na masuala ya udukuzi) lilisema kuwa liliweza kudukuwa akaunti ya Dropbox na Twitter ya Bw. Jack Dorsey(CEO wa Twitter) jambo liliongeza msukumo na kudai kuwa CEO wa Twitter anaweza kuona nyilwa za watumiaji wa mtandao ujulikanao kama ‘Vine’. Vine ilinunuliwa na Twitter mwaka 2012.
Tuliweza kudukua akaunti ya Bw. Jack na kuweza kuona vitu mbalimbali ikiweno picha iliyoko kwenye sehemu ya kurekebishia vitu mbalimbali(control panel) na kuweza kuona taarifa mbalimbali pamoja na passwords zao katika Vine.
Hata hivyo Twitter wamekanusha madai hayo na kusema kuwa Admin wa ‘Vine’ aliambiwa kuwa hairuhusiwi kuweza kufanya nennosiri ya mtumiaji wa mtandao huo (Vine) kuweza kuonekana katika hali yoyote ile na kuongeza kuwa passwords za watumiaji wa mtandao huo wanazitunza vizuri sana na daima zipo salama.
OurMine wameweza kudukua akaunti za mitandao ya kijamii za watu mbalimbali wakiwemo watu maarufu duniani kama Mark Zuckerberg na kuandika ujumbe katika ukurasa wake wa Twitter “Tunajaribu usalama katika mtandao wako” lengo la kuu likiwa ni kufanya watu waweze kuwa na uelewa kuhusu usalama katika intaneti.
Kitendo hicho cha akaunti za Bw. Jack pamoja na watu wengine maarufu duniani kudukuliwa kimezua maswali mengi na kuuliza kwanini Mkurugegenzi huyo mtendaji aliamua kuziacha taarifa mbalimbali zinazohusiana na mitandao ya kijamii wazi au hata kuzihifadhi katika ‘Dropbox?’.
Teknokona inakushauri kuwa na password ambayo ni ngumu kudukuliwa(strong password). Pia kuwa na tabia ya kubadilisha password hiyo mara kwa mara(baada ya miezi 3-6).
Soma Pia
- Jinsi ya kutengeneza password (nywila) imara
- Je ni sahihi ku’share password yako na mtu mwingine kama ndugu au mpenzi?
Makala hii imeandikwa kwa usaidizi wa karibu wa Tech Tines na Maine News Online