Twitter ni moja ya mitandao ya kijamii ambao umejikita zaidi kuhabarisha, kukutanisha na watu lakini katika mtindo wa kipekee kabisa kuanzia idaidi ya maneno kwa chapisho, muonekano wake na sasa inaboreshwa kutanua wigo wa watumiaji kuonyesha hisia zao.
Unachapisha kitu kwenye Twitter watu mbalimbali wanaweza kupendezwa na kile ambacho umekiweka hivyo basi idadi ya wanaume kwa wanawake waliovutiwa wataonekana tuu.
Katika kile ambacho kinapikwa kwenye Twitter wahusika wanaweka mambo sawa na kuongeza namna ambavyo watumiaji wa Twitter wanaweza kuonyesha hisia zao kwenye chapisho ambalo mtu ameliweka. Katika siku za usoni mtu ataweza kuonyesha ishara ya kufurahishwa kwa kucheka, huzuni, kuguna.
Twitter is working on Tweet Reactions view:
“Likes”, “Cheer”, “Hmm”, “Sad”, “Haha”
The icons for the Cheer and Sad reactions are WIP and shown as the generic heart one at the moment https://t.co/ZCBhH8z7JR pic.twitter.com/dGqq1CzIis
— Jane Manchun Wong (@wongmjane) May 28, 2021
Huu ni kama mwendelezo wa kuboresho vitu vya mtindo kwani mtandao huo wa kijamii ulishaongeza mtindo huo wa kuonyesha hisia kwenye uwanja wa kuandika ujumbe mfupi wa maandishi ambapo mtumiaji anaweza kuuweka kikatuni fulani kama ishara ya kufurahi, kupenda, kulia, kukasirika, n.k.
Maboresho haya yatakuwa sehemu ileile kama iliyo kwenye Facebook kwa maana ya kwamba kwenye kitufe cha “Like” (penda) kisha kuchagua kile ambacho ataona kinafaa kulingana na chapisho husika.
Unawaza kuhusu lini maboresho hayo yataanza kupatikana? Tutegemee kuona kitu hicho ndani ya wiki chache zijazo. Kuna mengi ambayo Twitter imeboresha na vingine kuwa vitu vipya kabisa. Je, unaizungumziaje Twitter ya sasa?
Vyanzo: The Verge, DNA India
No Comment! Be the first one.