Kwa kawaida Microsoft office huwa inauzwa kwa dola za kimarekani 70 kwa mwaka. Ni huduma ya kulipia kila baada ya muda Fulani.. yaani unapewa leseni ya kutumia ndani ya muda Fulani kisha unalipia tena ili kuendelea kutumia.
Microsoft Office ina program muhimu sana katika maisha ya kila siku. Leo TeknoKona inakuonyesha jinsi ya kupata Word, Excel, PowerPoint, na application zingine za Microsoft bila hata kulipia thumni.
Haitajalisha unatumia kompyuyta gani iwe PC ya windows 10 au hata Chromebook una uwezo wa kutumia Microsoft office ukiwa katika mtandao. Kwa kifupi huduma hii itakulazimu uwe katika mtandao ndio uitumie.
Kutumia kompyuta yako ingia katika mtandao wa Office.Com na kisha jiunge kwa ku ‘Sign In’ kwa kutumia akaunti ya Microsoft (kama huna, tengeneza).
Ukishaingia ndani click alama za Word, Excel, au PowerPoint ili kuanza kutumia. Kumbuka huduma hizi hazitaweza fanya kazi kama hakutakuwa na huduma ya kimtandao (intaneti). Kumbuka ukitumia kwa muundo huu kila kitu kinakuwa ni bure kabisaa…
One Comment
Comments are closed.