TCL kampuni ambayo wengi wanaifahamu kwa bidhaa za runinga janja lakini hata upande huu wa rununu wapo na wamekuwa wakitoa simu hizi za kisasa hivyo kuwafanya kuwa washindani. Mwezi huu wa Septemba wameamua kutoa simu janja TCL L10 Pro.
Septemba hii imeonekana kwamba isipite hivi hivi tuu bila ya TCL kutoa simu janja ya kwao ambayo kimsingi haina mengi; kwa lugha rahisi ni rununu ambayo inafaa kwa matumizi ya kawaida ambayo inafanya mtumiaji kuperuzi vizuri tuu mtandaoni pamoja na kutumia programu tumishi mbalimbali. Simu hii imezinduliwa huko Brazil na sifa zake ni hizi:
Kioo/Muonekano
Hapa unakutana na simu janja yenye kioo cha urefu wa inchi 6.22 aina ya LCD ambacho kina ung’avu wa hali ya juu (unaovutia) huku mwonekana wake wa mbele ukipendezeshwa na kamera ya mbele yenye MP 5, iliyoingia ndani kidogo mithili ya bonde.
Kamera/Memori
TCL L10 Pro ina kamera tatu nyuma ambazo zina MP 13, 5 na 2 halikdhalika zikiwa na taa ya kuongeza mwanga sehemu hafifu. Vilevile, RAM yake ni GB 4 kwa 128GB za diski uhifadhi.
Betri/Mengineyo
Betri ya kwenye simu hii ina uwezo wa 4000mAh, inatumia kadi mbili za simu, kipuri mama cha rununu husika ni Unisoc SC9863A, kasi ya intaneti inaenda mpaka 4G LTE, inakuja na Android 10, WiFi, Bluetooth 4.2 vipo.
No Comment! Be the first one.