Simu Janja siku hizi zinakuja huku zikiwa na maboresho ya hali ya juu; huyu akiweka kamera nzuri kampuni pinzani na yenyewe inafanya hivyo huku ikiongezea maboresho mengine.
Ni wazi kwamba simu za Samsung ndio zinazoongoza katika soko la dunia la simu. TECNO nao hawapo nyuma katika kuhakikisha wanampatia mteja kile kilicho bora zaidi.
Leo nataka kulinganisha simu hizi mbili kwa haraka haraka (TECNO Phantom 8 na Samsung Galaxy Note 8) ili ujionee yale yaliyomo ndani katika simu hizi.
Kilinganisho |
Phantom 8 |
Galaxy Note 8 |
RAM | GB 6 | GB 6 |
Mega Pixels (MP) | Kamera Ya Mbele 20MP, Yenye Flash Mbili na Kamera Ya Nyuma Ziko Mbili 12MP + 13MP, Uwezo Wa Kuzoom Mara 10 Zaidi | Kamera Ya Mbele 8MP na Kamera Ya Nyuma Ziko Mbili Zote Zikiwa Na 12MP lakini Kazi Ni Tofauti Tofauti. |
Kamera Mbili? | Ndio – Nyuma Ziko Mbili | Ndio – Nyuma Ziko Mbili |
Uwezo Wa Betri | 3,500mAh – Haliwezi Toka | 3,300mAh – Haliwezi Toka |
Prosesa | Octa core 2.6 GHz | Octa-core (2.3GHz Quad +1.7GHz Quad), 64-bit, 10nm processor |
Network | Inaruhusu Mpaka 4G | Inaruhusu Mpaka 4G |
Ujazo Wa Ndani (ROM) | GB 64 | GB 64 |
Memori Kadi? | Inaruhusu Kuongeza Mpaka TB 2 | Inaruhusu Kuongeza Mpaka GB 256 |
Uwezo Wa Kioo | 1920*1080 FHD | 1440 x 2960 pixels |
Aina Ya Kioo | IPS (LCD) | AMOLED |
Ukubwa Wa Kioo | Inchi 5.7 | Inchi 6.3 |
Utambuzi Wa Alama Za Vidole? | Ndio – Upo Kwa Nyuma | Ndio – Upo Kwa Nyuma |
Rangi Zilizopo | Champagne Gold, Phantom Black Na Galaxy Blue | |
Ukubwa (Wembamba) | 159.95 x 79.5 x 7,9 mm (wembamba 5.6mm) | 162.5 x 74.8 x 8.6 mm (6.40 x 2.94 x 0.34 in) |
Jumba Lake | Kioo Kikubwa Ambacho Kimezungukwa Na Umbo bapa la chuma | Nyuma Na Mbele Kuna Kioo (Gorilla Glass 5) Pia Imezungukwa Na Fremu Ya Aluminiam. |
Ukizitazama sifa za simu hizi mbili kwa umakini kabisa na kulingana na thamani ya pesa yako nina imani utajua kabisa ni ipi ya kuinunua.