Tumetoka mbali na teknolojia na kwa hakika kuna watu sasa hivi wamesahau tabu ya kutaka kujua namba inayompigia namba ni ya nani (iwapo haijaihifadhi kwenye simu).
TrueCaller ni app maarufu duniani inayowawezesha watumiaji wake kutambua majina ya watu au makampuni wanayotaka kuwasiliana nayo au yanayowapigia simu wao. Kwa kifupi, mtumiaji wa TrueCaller anaweza kufahamu jina la mtu au kampuni kabla ya kupiga au kopokea simu.
Mfumo wa data wa TrueCaller ni mfumo unaofahamika kama ‘Crowdsource‘. Yaani watumiaji wake wanasaidiana kupeana taarifa za data za watu waliokwenye simu zao.
Unapopkua programu hiyo kutoka kwenye Playstore/App Store kisha ukaingia ndani kwa kuweka barua pepe na nywila basi utakuwa umeruhusu wahusika kuona namba za watu ulionao kwenye kifaa husika na kuhifadhi taarifa hizo na kwenye kompyuta zao za kutunza kumbukumbu (servers).
Sasa pale mtu anapokupigia simu huku ukiwa umeruhusu huduma ya intaneti app ya TrueCaller italinganisha namba hiyo pamoja na kumbukumbu za watumiaji wengine wa programu hiyo na kutoa jina pamoja na taarifa nyingine mathalani namba hiyo imesajiliwa nchi gani.
Hivi ndiyo jinsi app hii inafanya kazi.
Changamoto:
Changamoto kubwa ni mtazamo wa watu ambao hawapendi au kuamini katika kuachia taarifa zao (data – za namba za simu) kwa huduma za kimtandao.
TrueCaller ni huduma kutoka taifa la linalosifika katika ulindaji wa data za watumiaji wa huduma katika biashara zake – Swideni. Jambo hili limehakikisha katika miaka mingi hadi sasa TrueCaller imeendelea kutoa huduma hii bila skendo kubwa ya suala la usalama wa data.