Kufuatia kuhairishwa kwa mashindano ya Olimpiki mwaka jana Samsung ambao pia ni wabia walishindwa kutoa toleo maalum la simu janja kama njia ya wao kujitangaza kwa watu kutoka mataifa mbalimbali duniani.
Waandaji wa mashindano ya Tokyo Olimpiki 2020 mwaka huu wamedhamiria yafanyika na hivi sasa yapo katika hatua ya majaribio na tarehe (Julai 23-Agosti 8 2021) iliyopangwa kufanyika haijabadilishwa. Samsung nao wanajiweka tayari kutoa simu janja maalum kabisa kwa ajili ya mashindano hayo.
Inaelezwa kuwa toleo maalum la Samsung Galaxy S21 kwa ajili ya mashindano ya Tokyo Olimpiki 2020 lipo tayri ambapo simu hiyo imenakshiwa kwa rangi, picha zinazohusiana na shughuli hiyo nzima. Kwa uchache tuu simu hiyo ina kioo chenye urefu wa inchi 6.2. kipuri mama ni Snapdragon 888 na ukubwa wa diski uhifadhi ni GB 256.
Kuna mengi ambayo toleo hilo maalum inafanana na ile ambayo sote tunalifahamu mathalani sifa za kamera kwenye Galaxy S21 kwa ajili ya mashindano ya Olimpiki nni sawa kabisa na toleo mama. BOFYA HAPA kufahamu undani wa simu janja Samsung Galaxy S21.
Simu hiyo inaelezwa huenda ikatoka mwezi Juni mwaka huu lakini bei yake bado haijawekwa wazi. Tuambie ewe msomaji wetu wa kila siku, unaizungumziaji habari hii?
Vyanzo: Engadget, Android Authority
2 Comments