Wapenzi wa kucheza magemu iwe kwa njia ya mtandao au hata kwa kifaa kingine cha kidijitali naamini tunafahamu gemu la Call of Duty ambalo limekuwepo kwa miaka mingi sasa na limekuwa likiboreshwa kila toleo jipya ambalo linatoka.
Tangu mwaka 2003 hadi leo hii bado gemu la Call of Duty lipo kwenye ushindani na likiwa na wapenzi lukuki duniani kote. Gemu hili ambalo ni la mambo ya kivita kivita limekuwa kipenzi cha wengi kwa karibu miaka 20 sasa lakini huenda baada ya toleo la mwaka huu kutoka tukapumzika kwa maka kabla ya nyingine kuletwa.
Taarifa hii inaweza isiwe nzuri hasa kwa wapenzi wa gemu husika lakini sababu kubwa ya kufikiria kuchelewesha kutoa toleo litakalotoka baada ya mwaka huu ni kutokanana mauzo ya Call of Duty Vanguard kutofikia malengo lakini pia mabosi wanaamini utoaji wa magemu mengi haraka haraka mfano Black Ops Cold War imemeza mahitaji ya toleo jipya.
Njia ya hawa wanaotengeneza magemu kupata pesa ni kwa kuuza bidhaa zao ambapo unakuta toleo linalotoka linakuwa katika aina mbili tofauti; moja haihitaji mtu kulipia ili kulicheza na jingine linakuwa lazima ulipia kiasi fulani cha pesa ili kuweza kuburudika.
Toleo la Warzone ambalo si la kulipia limeathiri mauzo ya jumla ya gemu husika na katika kipindi ambacho Call of Duty itakuwa haipo zitakuwepo vitu ambavyo zitaziba kutokuwepo kwa toleo jipya zikihusisha uwezo wa kucheza bure na ile ya kulipia.
Toleo lijalo la gemu husika linategemea kutoka karibu kabisa na mwisho wa mwaka 2022 hivyo wapenzi wa magemu inabidi waendelee kufurahia kilichopo na hayo mapya ambayo yatakuwa yanatoka.
Vyanzo: Engadget, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.