Nadhani umeshasikia kuhusina na mvutano kati ya wasanii wawili (Timbaland na Swizz Beatz) na mtandoa wa kijamii wa Triller.
Triller ni moja kati ya washindani wakubwa sana wa mtandao wa TikTok, miezi kadhaa nyuma wasanii hao wawili walisema wajalipwa madola ya mamilioni baada ya kuuza kampuni yao ya Verzuz kwa kampuni hiyo mwaka jana.
Malipo hayo yalipangwa kulipwa kwa awamu tofauti tofauti, na mwezi uliopita wasanii hao wawili walifungua mashtaka na wakitaka walipwe dola milioni 28 za kimarekani na Triller.
Kwa sasa vyanzo vinasema kuwa kampuni hiyo imefanya busara na kuweza kufikia muafaka na wasanii hao wawili kisheria maana jambo lilikua likienda hivyo.
Kingine ni kwamba hakuna taarifa kamili ambayo imeachiwa wazi kama wamefanyiwa jambo gani na kampuni hiyo, na je kama ni malipo ya pesa wamelipwa sh. Ngapi?
Kwa haraka haraka kilichotokea ni kwamba kampuni ya Triller ilibidi kutoa dola milioni 18 mpaka kufikia machi 20 na kisha kuanza kulipa dola milioni moja kila mwezi kwa miezi kumi ili kufikia dola za kimarekani milioni 28.
Shitaka lililokuwepo ni kwmaba kampuni hiyo haikufanya hvyo, japokuwa wenyewe Triller wanasema wamefanya nusu ya hivyo lakini hapo kwenye dola milioni moja moja kwa mwezi ndio kuna viulizo.
Kwetu hili ni jambo zuri kama wenyewe wamefeikia muafaka, yaani pande zote mbili zimetoka zikiwa na Amani ya kile kilichofanyika
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je umeipokeaje hii kwa kampuni na hawa jamaa kufikia muafaka?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.