Lenovo wametambulisha laptop mpya inayokwenda kwa jina la ThinkPad X1 Fold laptop yenye skrini yenye uwezo wa kukunjwa.
Laptop hii inayotumia programu endeshaji ya Windows 10, inachukua sifa ya kuwa laptop ya kwanza kuja na teknolojia hii ambayo tayari imeanza kuja kwenye simu – kama vile Samsung Galaxy Fold.
Laptop hii inaweza kutumika kama tableti lakini pia inaweza kutumika kama kompyuta kamili kutokana na uwezo wa kutumia keyboard za mfumo wa bluetooth. Inaukubwa wa inchi 13.
Sifa na uwezo wake
- Inakuja prosesa ya Intel Lakefield
- Port mbili za USB-C
- Uwezo wa kutumia laini (Sim Card)
- Uwezo wa RAM wa GB 8
- Uwezo wa Diski Uhifadhi wa TB 1
- Uzito wa takribani kilogramu 1.1
- Teknlojia ya 5G
Laptop ya ThinkPad X1 Fold imeanza kupatikana kwa malipo ya awali (preorder) ya dola 2,499 (Zaidi ya Tsh Milioni 5 za kitanzania).
Vyanzo: The Verge, Lenovo na tovuti mbalimbali
No Comment! Be the first one.