Zipo tetesi katika mitandao ya teknolojia kwamba kampuni ya Google ipo mbioni kuachia app yake mpya ya Allo ambayo ni kwaajiri ya kutuma ujumbe ambayo ilitangazwa katika mkutano wa waandaji Google I/O uliofanyika mwezi Mei mwaka huu.
Google Allo ni app kwaajiri ya kuchati kama vile zilivo app za Hangouts na messenger ambazo pia zinatengenezwa na Google lakini app hii inakuja na uwezo maalumu wa kujifunza tabia yako na namna unayojibu meseji zako hivyo kukusaidia kujibu meseji.
Allo itakuja na uwezo wa mkubwa wa kujifunza kile tabia zako za uandishi wa ujumbe, utalaamu huu ambao kwa kingereza unaitwa Machine learning unaifanya app hii kujifunza namna ambayo unajibu jumbe zako na hivyo baada ya muda mrefu wa kujifunza itaweza kujibu baadhi ya meseji kutoka kwa marafiki zako bila wewe kuandika kitu.
Google allo hata hivyo ni wazi haitaelewa lugha isiyo rasmi hii ni pamoja na kiswahili ama kingereza kisicho rasmi yaani lugha ya ufupisho ambayo inatumika zaidi katika mitandao. Kwa mtazamo wa haraka haraka app hii itapata shida kufikia malengo kwa watumiaji vijana wa karne hii.
Hii ni changamoto kwa waandaaji wa app na programu za kompyuta kuangalia katika eneo la Machine learning na kulifanyia kazi eneo hili la sekta ya teknolojia.
Wegi wanasubiria hii app kwa hamu ili kujionea ni kiasi gani inaweza kuwa na msaada hasa kwa watumiaji wa kawaida! Tayari app hii imepewa nyota 4.9 na walio ijaribu katika soko la Google play kama inavyoonekana katika picha hapo juu.