Tesla ni kampuni kubwa sana inayojihusisha na kutengeneza magari ambao yanatumia umeme. Kitu ambacho kimeshangaza wengi ni kwamba kampuni hiyo inafikiria kuanzisha huduma ya muziki wa ku’stream.
Apple Music na Spotify pamoja na makampuni mengine inabidi yajiandae kwani yanaweza yakawa yamepata mpinzani mkubwa.
Tesla kwa upande wao inasemekana kuwa kama teknolojia hii ikifanikiwa basi itakua ni msaada mkubwa kwani lengo lake kubwa ni kutumika katika magari — yaani huduma hii ya ku’strem itakuwa inapatikana katika magari == kutoka Tesla.
Taarifa zilizopo ni kwamba kampuni hiyo imeshaongea na lebo kubwa mbalimbali katika maswala ya muziki na hii ni kuonyesha tuu ni jinsi gani kampuni iko makini na kile inachotaka kukifanya.
Kwa haraka haraka, Tesla atakua ni mshindani mkubwa wa Apple Music na Spotify kwa sababu anaanzisha huduma yake ya muziki wa ku’strem
Hakufikiria kuweka huduma ya Apple Music au Spotify katika magari yake kwani alijua kunaweza kukawa hakuna maelewano mbeleni (katika ya Tesla, lebo. na kampuni la huduma n.k). Ili kuliepuka hilo ni kuanzisha kampuni lako mwenyewe
Na ukianzisha kampuni lako hakuna lebo inaweza ikakukataa kwani jambo hili linawaongezea sana mapato kama kampuni.