Kumekucha…kumekucha…. Telegram na Apple wararuana tena na sababu ikiwa ni kwamba Telegram inadai kuwa Apple inazuia Sasisho (Update) yake kuhakikiwa haraka.
Kilichotokea hapa ni kwamba, mtandao wa Telegram wako na toleo lao jipya la App yao na kwa kawaida kwa kampuni ikiwa katika hali hii lazima itume sasisho hilo kwa Apple wenyewe
Kabla ya sasisho hilo halijawekwa ili watu waweze kulishusha lazima Apple walifanyie uhakiki kama liko sawa…hapa ndipo kunapoleta utata sasa.
Mtandao hup unadai kuwa wameshafanya kila ambalo wanahitajika kulifanya na zoezi lililobakia ni kampuni ya Apple kupita AppStore kuhakiki tuu sasisho hilo ili liweze kuwafikai watu.
Mkurugenzi mkuu wa kampuni, bwana Pavel Durov anadai kuwa toleo hilo jipya linaenda kabisa kubadilisha na kuleta mapinduzi makubwa katika swala zima la huduma ya kutuma na kupekea ujumbe lakini Apple bado hawajaidhinishi.
Bado toleo hilo jipya halijafahamika litakua limebeba vitu gani ambavyo katika katika toleo la nyuma havikuwepo.
Lakini hii sio mara ya kwanza kwa wawili hawa kuingia katika sakata kama hili hata mwaka 2018 jambo kama hili lilitokea.
Kwa sasa pia kuna huduma ya Telegram ya kulipia inayojulikana kama Telegram Premium ambayo ni dola za kimarekani 5 kwa mwezi.
Kupitia huduma hiyo unaweza kupata uwezo wa kupandisha na kushusha mafaili makubwa zaidi, ushushaji wa haraka zaidi, uwezo wa kutamka maneno yakajiandika yenyewe, emoji za pekee na mengine mengi.
Ningependa kusikia kutoka kwako, hebu niandikie hapo chini katika eneo la comment, je unadhani Apple wanafanya makusudi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.