Shirika la ndege la Rwanda, Rwandair, limezidisha ushindani katika uchukuzi wa ndege Afrika Mashariki na Kati kwa kununua ndege aina ya Airbus A300-200 iliyoitwa “Ubumwe” (Umoja).
Ndege hiyo ilizinduliwa kwa mara ya kwanza kwenye uwanja wa kimataifa wa Kanombe, Kigali. Kabla ya kufika Kigali, ndege hiyo ilitua uwanja wa ndege Entebe na kupokewa na viongozi ya kidiplomasia pamoja na mapokezi ya hadhi ya juu kwa ndege mpya. Hivyo basi ndege hiyo itawezesha shirika hilo kufika masoko ya Ulaya na bara Asia.
Ukiwa angani ndani ya ndege hii unaweza kupiga simu, kupata ujumbe wako wa simu, ujumbe wa barua pepe, ujumbe wa WhatsApp na mawasiliano mengine na kabla ya ndege hiyo hakukuwepo ndege nyingine yoyote yenye uwezo huo.
Ni ndege iliyotengenezwa nchini Ufaransa na kununuliwa kwa kitita cha dola milioni 200 za marekani|zaidi ya Tsh bil. 436.8. Ndege hiyo inaifanya Rwanda mpaka sasa kuwa na ndege 9 na nne nyingine zikitarajiwa kufika mwishoni mwa mwezi Feb mwakani.
Safari ya kwanza ya ndege hiyo inatarajiwa kufanyika wikendi ijayo tarehe 8 Oktoba kuelekea mjini Dubai. Mbali na Rwanda hakuna nchini nyingine yoyote katika ukanda wa Afrika Mashariki/barani Afrika yenye ndege kama hiyo.
Una maoni yoyote kuhususiana na hili? Niandikie maoni yako katika sehemu ya comment.
Kumbuka kusambaza makala na pia kuungana nasi kupitia Facebook, Twitter, Instagram, YouTube, Telegram na Google Plus
Vyanzo: BBC, newtimes.co.rw