Teknolojia ya magari ya umeme kwa ajili kutoa huduma za utalii imetambulishwa rasmi kwenye Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Teknolojia hiyo inatajwa kuwa rafiki wa mazingira na uhifadhi kwa kuwa magari hayo hayana kelele za ngurumo sanjari na ukweli kwamba hayatoi moshi kama ilivyozoeleka kwa magari mengine yanayotumia mafuta.
Hayo yamebainika baada ya Kampuni ya Mount Kilimanjaro Safari Club inayojishughulisha na utoaji wa huduma za utalii kutambulisha teknolojia hiyo kwa kuanza na magari mawili na imesema katika hatua za awali imeonyesha mafanikio makubwa.