Inafahamika kuwa OnePlus ni kampuni kubwa ambayo inajulikana katika soko la simu janja. Kampuni imejibebea umaarufu mkubwa baada ya kutoa simu janja zake ambazo zina hadhi ya juu na pia zinaweza kushindanishwa na simu zingine.
Teknolojia ya simu inabadilika sana, kumbuka Samsung wanakuja na simu janja ambayo inakunjika (foldable). kwa upande wa OnePlus wao hawana papara kabisa na jambo hili ….. ndio kwanza wanafikiria vitu vingine kabisa.
Mkurugenzi mkuu wa OnePlus, Pete Lau amesema kwamba “Simu za kujikunja skrini sio sahihi sana kutoka kwa kipindi hichi kwani hakuna kitu ambacho ni kikubwa sana inachofanya ambacho ni tofauti na simu za kawaida…. ukiachilia mbali bei”
Hivyo basi kampuni inafikiria mambo mengine kede kede ambayo itawafanya kwa namna moja au nyingine kujitanua katika biashara. Hii inamaanisha ni pamoja na kuanzisha bidhaa zingine kama vile, Magari ya umeme, Tv janja na mengine mengi,
Maeneno hayo alisema wakati anahutubia katika chuo cha European Institute of Design, huko Italy. Hapa alijaribu kuelezea mambo ambayo wanayategemea mbeleni katika kampuni ya OnePlus.
Bado alisisitiza kuwa kuna uwezekano mkubwa kampuni ikaanza kutengenza vifaa vya kiletroniki kwa ajili ya ofisi ambavyo kwa ujumla vitakua na teknolojia ya 5G na AI.
Tv iko mbioni kutangazwa rasmi lakini biashara nyingine kama magari zitachukua muda kidogo, vile vile kutengeneza na kuuza simu kupo pale pale.