TECNO ni moja kati ya makampuni makubwa ya kuuza na kutengeneza simu. Ni wazi kwa china bado kampuni ipo katika nafasi za juu kabisa katika makampuni ambayo yanazalisha simu janja
Ni sawa soko lake kubwa kabisa ni Afrika, na bado wigo huo unazidi kutanuka maana walivyoanza walianza na Afrika tuu ndio hapo baadae wakaenda ulimwenguni kote.
Tukiongelea ulimwenguni kote, kwa sasa wamejisogeza karibu nchini Uturuki, katika mji mkuu wa nchi hiyo (Istanbul). Katika nchi hiyo wanafungua uwekezaji mkubwa wa kiwanda na wana mpango wa kuajiri wafanyakazi wasiopungua 1,000
Kumbuka tangia mwaka 2016 mwishoni TECNO ilianza rasmi kuidhamini timu ya mpira wa miguu ya Manchester City, hii ikiwa ni moja kati ya kampeni zake za kukua na kujitangaza zaidi.
Ni wazi TECNO inasema kuwa unevutiwa zaudi na serekali ya Uturuki kupitia katika sera zake za uwekezaji na hizo ndizo zimeifanya kampuni kwenda kuwekeza nchini humo.
Mpaka sasa TECNO iko katika zaidi ya masoko 60 ya kuuza na kutengeneza simu janja, hii ni dalili nzuri ya kuonyesha kuwa kampuni ya TECNO inapambana vikali ili kuhakikisha inazidi kushika katika nafasi nzuri (katika soko la aina hii).
Ni pongezi kubwa kwa kampuni hiyo maana inazidi kupanua wigo wake, TekoKona Tunatoa pongezi!
Kumbuka Kutembelea Mtandoa Wako Pendwa Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
No Comment! Be the first one.