Soko la simu limekuwa limekuwa na ushindani mkubwa na kupelekea makampuni ya simu kuja na mbinu mpya za kujizolea wateja. Tukiongelea makampuni pendwa ya simu Afrika hatuezi kuacha kuipongeza kampuni ya simu ya TECNO.
Tunafahamu TECNO ina matoleo mbalimbali kama vile phantom, Camon, L series, Spark Series na mengineyo, na yote ni matoleo pendwa kutokana kuwa na sifa zenye kuvutia kama vile kamera nzuri, battery kubwa. lakini kati ya matoleo yote toleo la Spark limeonekana kupendwa sana labda hii ni kutokana muonekano mkubwa, utendaji maridhawa na bei isiyomuumiza mteja.
Pengine msomaji unaweza kujiuliza kwanini nmeamua kuizungumzia TECNO hususani TECNO Spark 5 pro ambayo ipo mbioni kuja na kwanini tutaepukana na ununuzi wa memori ya ziada ili kukidhi mahitaji yako.
Nikiwa kama mfuatiliaji wa masuala ya teknolojia na simu janja kwa ujumla nikapata wasaa wa kutembelea kwenye ukurasa wa Instagram- @tecnomobiletanzania na kukutana na picha ya Spark 5 pro yenye sifa zenye kuonekanika kama kioo aina ya Dot in Display cha takribani nchi 6 au 7 si chini ya hapo, nyuma ikiwa na kamera 4(16MP+2MP+2MP+AI Lens) na MP 8 za selfie. Kutokana na sifa hizo chache TECNO Spark 5pro ni mkali wa Spark zote za awali.
Katika siku za usoni tutaleta uchambuzi kuhusu Tecno Spark 5 Pro na endelea kutufuatilia kila inapoitwa leo kwa habari mbalimbali zinazohusu masuala ya teknolojia.
Chanzo: Tecno
No Comment! Be the first one.