Sakata la kuonyesha chaneli za ndani bila ya wateja kulipia limefikia sehemu ambayo mpaka serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoa neno.
Dk Harrison Mwakyembe (Waziri) ameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kutoa mwongozo utakaowezesha kampuni zilizokiuka masharti kuweza kurejea kuonyesha ya chaneli za ndani kama ilivyokuwa hapo awali.
Kampuni zilipewa leseni ya kuonyesha chaneli za kulipia lakini zikaingilia soko la wenzao kinyume cha utaratibu wa leseni zao. Inaelekea hawa wenzetu wanapenda kurusha haya maudhui ya chaneli za ndani, hivyo TCRA itoe mwongozo wa nini wafanye ili kuendelea kutoa huduma~Dk. Mwakyembe.