Ni wazi kumekuwa na malalamiko mengi sana kuhusiana na bando za simu. Malalamiko mengi yamekuwa yakihusina na bando la internet.. kwamba wateja wanaweka bando hizo na zinawahi kuisha. TCRA na wizara husika zina tamko gani?
Malalamiko hayo hayo yamekuwa yakihusisha makampuni yanayotoa huduma hizo (mfano tigo, airtel, halotel n.k). Watumaiji wamekua wakilalamika kwamba wanaibiwa aidha ikiwa kwa njia ya vifurushi vyao kuisha katika hali ya sintofahamu
Ukiachana na hayo kuna muda huduma inakua mbovu kiasi kwamba halii inapelekea bando kuisha muda wake wa kutumiwa bila hata ya mteja kutolitumia
Kingine ni kwamba bado kuna malalamiko kwamba makampuni hayo yanatoza gharama kubwa katika vifurushi vya intaneti na hata vile vya kupiga na kupokea simu (ongezeko hili hata mimi nimeliona ahahaha!)
Waziri wa mawasiliano na teknolojia ya habari Dk. Faustine Ndugulile ametoa elekezo kwa mamlaka ya mawasiliano na habari TCRA kwamba jambo hili lipatiwe muarobaini mapema sana
Waziri pia amesema kuwa inabidi TRCA ianzishe mfumo wa uhakika na shutuma hizo kwa kufuatilia gharama wa kujua gharama halisi ya mawasiliano na kiasi ambacho wateja wanalipia.
Watanzania sio wajinga, wanahitaji kujua thamani ya pesa zao katika bando hizo” —- aliendelea kusema waziri
Kingine cha kushangaza ni kuwa katika repoti iliyotolewa na ‘ICT Africa Internet’ inasema kuwa Tanzania ndio nchi ambayo ina gharama ndogo katika bando za intenet kwa africa mashariki.
Somo Zaidi Habari Za TRCRA hapa!
Vyanzo ni DailyNews & Allafrica
No Comment! Be the first one.