Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesitisha utoaji wa leseni mpya za maudhui ya mtandaoni ili kujipa muda wa kufanya tathmini na maboresho ya utaratibu huo.
Teknolojia inakuwa kwa kasi sana duniani kote kitu ambacho kinaenda sambamba na suala zima la utandawazi ambapo hivi leo kuna tovuti nyingi tuu za kuhabarisha, runinga za mtandaoni, n.k. Katika suala zima la maudhui TCRA wamekuwa wafuatiliaji wazuri tuu katika kuhakikishamiongozo waliyoiweka kuhusu kile kinachokwenda mtandaoni basi kiwe kinatoka kwa mtu wanayemtambua kwa maana ya kwamba mhusika awe na leseni inayomruhusu kufanya kazi husika.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Mkuu wa TCRA Kanda ya Ziwa, Mhandisi Mihayo wakati wa tafrija ya “Usiku wa waandishi wa habari/wadau wa habari kanda ya ziwa” kwa kusema mamlaka hiyo imesitisha utoaji wa leseni mpya za maudhui ya mtandaoni tangu Januri 28 2021 hadi Juni 30 2021.
Swali la kujiuliza nini kiini cha TCRA kufikia uamuzi huo?
Ni suala ambalo utakubaliana na mimi kuwa utandawazi umesababisha mambo mengi kukiukwa kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo TCRA uamuzi huo umetokana na kuendelea kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa matumizi sahihi ya mtandao.
Sasa ni wakati wa sisi ambao tunapenda kuwa na runinga za mtandaoni, tovuti za upashanaji habari kukaa zinazotambulika na mamlaka kukaa mkao wa kula kusubiri maboresho ambayo TCRA watakuja nayo Juni 30 2021.
Vyanzo: TCRA, Malunde.
One Comment