Watumiaji wa Instagram tufahamu hili kuwa siku si nyingi itakuwa ni lazima kujaza tarehe ya kuzaliwa kwenye akaunti ya mtumiaji. Hii inatazamiwa kuja katika siku za usoni ikiwa inalenga kitu fulani.
Instagram ambayo ina watumiaji lukuki duniani kote kiasi kwamba kwa wengine imeshakuwa uraibu kwa maana ya kwamba kila baada ya muda fulani ni lazima waperuzi huko lakini kwa upande mwingine imekuwa chanzo cha mapato kwa watu mbalimbali kutokana na kile ambacho wanakiweka huko.
Kwa muda mrefu kipengle cha kujaza tarehe ya kuzaliwa kwenye akaunti zetu za Instagram imekuwa si lazima; kwa maana ya kwamba hata mhusika asipojaza haina madhara hadi kumfanya mtu asiweze kuhifadhi taarifa zake. Lakini hilo sasa linaweza likabadilika siku si nyingi kwani kuna mpango wa kukifanya kipengele hicho kuwa ni lazima kujazwa (hakiwezi kuachwa wazi).
Lengo la kufanya hivyo ni kuwalinda wale walio chini ya umri wa miaka 18 kuwepo huko ambapo kwenye mitandao ya kijamii kuna mengi ambayo yanaweza kumfanya mtoto akaharibikiwa kutokana na utandawazi.
Instagram wanapanga kulitekeleza hilo kwa kuweka ujumbe amabao utaonekana kwa juu kabisa kwa yeyote ambae hakujaza tarehe ya kuzaliwa mara tu mtu atakapofungua kuperuzi kwenye programu tumishi husika. Iwapo mtu atakaidi kuweka kinahitajika basi chapisho lake halitaendampaka atakakupokuwa amejaza alichoambiwa aweke.
Haya sasa wewe msomaji wetu unafikiri kwa hatua hii itakusukuma kuweka kile ambacho Instagram wanakihitaji kutoka kwako? Unafikiri kwa hatua hii watafanikiwa kuwalinda wanaokusudiwa? Tunakaribisha maoni yako.
Vyanzo: Gadgets 360, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.