Simu zetu zinatumika katika kufanikisha mambo mbalimbali katika dunia ya leo na kwa wengine inaweza ikaonekana ni dharau lakini nchini Saudia mahakama imeridhia talaka kwa njia ya simu.
Wakati fulani nilishawahi kuandika kuhusu marufuku kutoa TALAKA kwa njia ya simu huko Tanzania Zanzibar lakini kwa nchi kama Saudia Arabia imeonekana kuwa itasaidia kuwaokoa watalakiwa.
Kwanini utoaji wa talaka umeruhusiwa nchini Saudia?
Nchini humo (Saudia Arabia) kabla ya sheria ya utoji talaka kwa njia ya simu (ujumbe mfupi wa maandishi) kupewa baraka na mahakama iliwezekana kupewa talaka ya siri jambo ambalo lilimfanya mwanamke kutojua kama ameshatalakiwa na hivyo kushindwa kudai haki zake.
Kujua kuwa mwanamke amepewa talaka kwa njia ya simu itasaidia?
Kwa mujibu wa wanawake, wanasheria wanawake waliokuwa wanapigania sheria hiyo ipite wamesema kuwa njia hiyo ya kumtaarifu mwanamke kuwa ametalakiwa itamsaidia kuwa na ushahidi ambao utamuweka katika nafasi ya kuweza kudai haki yake kwa muda wote alioishi na huyo mwanaume.
Sheria hiyo ilipata msukumo mkubwa wa kupitishwa/kukubaliwa baada ya kuwepo malalamiko mengi yaliyopo mahakamani kuhusu mwanamke kupewa talaka bila kujua.
Vyanzo: The Times of ISrael, Khaleed Times