#TAIC2021 – Tanzania Annual ICT Conference, ni mkutano unaofanyika kila mwaka ukiwaleta pamoja wadau mbalimbali wa sekta ya TEHAMA nchini kuzungumzia changamoto na fursa mbalimbali zilizopo kwenye sekta hii. Kwa mwaka 2021 kongamano hilo linafanyika hapa jijini Arusha.
Teknokona, kupitia kampuni mama, Teknokona Group tunafuraha kuendelea kuwa wadau muhimu wa kongamano hili. Kongamano limeanza leo tarehe 20, na kilele ni Ijumaa, 22 Oktoba.
Kauli mbiu ya #TAIC2021 mwaka huu ni “Kujenga Taifa la Kidigitali” na mgeni rasmi atakuwa Mh. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB), Waziri Mkuu wa JMT.
Furatilia yanayoendelea kwa urahisi kupitia ukurasa wa tume ya TEHAMA (ICTC), pia kumbuka kila siku utaweza kufuatlia mkutano huu moja kwa moja kupitia ukurasa wa ICTC.
ICTC YouTube – https://www.youtube.com/channel/UC-jrMbjRPayymcaY6KuYAzw
No Comment! Be the first one.