WhatsApp huwa wanatoa maboresho au vipengele vipya mara kwa mara katiaka kuhakikisha kuwa wanazidi kuwapa watumiaji wake kile wachostahili na si kingine bali huduma nzuri.
Kwa sasa mtandao wa WhatsApp unafanyia majaribio kipengele hicho cha kuwezesha mtumiaji kuweza kutafuta meseji za nyuma kwa kutumia tarehe.
Kama kipengele hiki kikitoka basi kwa watumiaji wa iPhone wataweza kukitumia kwa kwenda katika sehemu ya ‘Search’ katika uwanja wa ‘chat’ husika na kisha itaonekana alama ya kalenda pembeni kidogo ya ‘keyboard’
Ukiingia katika kalenda hiyo utakua na uwezo wa kuchakua mwezi siku na mwaka ambao unataka kutafuta meseji husika.
Hii itafaa zaidi kwa wale ambao wana mazungumzo mengi katika vifaa vyao, hata hivyo ukiachana na kipengele hiki bado katika eneo la ujazo uhifadhi ndani ya WhatsApp litakau limegfanyiwa maboresho pia.
Hapa kutakua na mpangilio wa kuendana na makundi mawili yaaani ‘Large Files’ na ‘Forwaded Files’ ambapo hapo unaweza ingia katika eneo mojawapo na kuweza kufanya unachotaka kama vile kufuta baadhi ya mafaili n.k.
Vipengele hivi viwili ni vya muhimu sana kuwa navyo haswa kama ni mtu wa kupokea jumbe nyingi, fikiria kwa wale wanaondesha biashara kwa kutumia mtandao wa WhatsApp, vipengele hivi vitakua ni msaada mkubwa sana sio?
Kwa sasa vipengele hivi havijaanza kupatikana rasmi maana viko katika hatua ya majaribio lakini vitaanza kupatikana hivi karibuni hivyo inabidi kuhakikisha unatumia toleo jipya kabisa la mtandao wa WhatsApp.
Niandikie hapo chini katika eneo la comment, je unaipa asilimia ngapi kampuni ya WhatsApp kwa kufikiria na kipengele hichi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.