Ile app inayotumika kumrahisishia mtumiaji wakati wa kuandika kitu kwenye simu janja imevujisha barua pepe wakati ikifanya kazi ya kumrahisishia mtumiaji kuotea kile anachotaka kuandika.
Wiki iliyopita watumiaji wa app hiyo walishangaa kuona maneno ambayo hajawahi kuyatumia hata siku moja kutokea katika harakati za kumrahisishia mtumiaji kwa kuotea kile anachotaka kukiandika; taarifa hizo zilijumuisha barua pepe za watu, namba za simu na hata app hiyo kutafasiri lugha ambayo mhusika haielewi hata kidogo.
Baadhi ya watumiaji wa app hiyo waliripoti kutofahamu barua pepe zinazoonekana wakati wakitaka ku-login na hata wengine kupigiwa simu na watu wasiowafahamu baada ya namba zao kuvuja kupitia SwiftKey app na hivyo kusababisha karaha kwa wateja wake.
Kitendo hicho kilileta karaha kwa wengi kwani app hiyo ilisababisha usumbufu kwa namna moja au nyingine. Hata hivyo SwiftKey wamesema kuwa usumbufu huo uliwapata watu wachache tu na tayari wameshaanza kulishughulikia tayari. Wameamua kuondoa huduma ya uwezo wa app hiyo kujua barua pepe ya mtumiaji.
Je, na wewe pia ulikumbwa na maswahibu hayo kutoka kwenye app ijulikanayo kama SwiftKey? Tuambie maoni yako katika sehemu ya comment hapo chini.
Endelea kufuatilia TeknoKona kila siku kwa kusoma makala mbalimbali.
Vyanzo: Engadget, The Verge