Pengine Sweden ndio inaweza ikawa nchi ya kwanza kuja na teknolojia hii kwa magari makubwa. Magara haya yanatembea katika barabara ambazo zimeunganishwa na nyaya za umeme
Kilichofanyika ni kwamba magari hayo kwa juu yameunganishwa na nyanya ambazo zinaelea (zilizo shikiliwa na nguzo). Jina la kitaalamu ya barabara hii ni eHighway.
Magari ambayo yanapita katika barabara hiyo ni yale makubwa kabisa na kwa sasa magari makubwa ya kampuni ya Scania ndio yanafanya majaribio katika barabara hizo
Inasemekana kuwa wakati yakiwa katika barabara hiyo yatakuwa hawayatumii mafuta hata kidogo, lakini yakitoka nje ya barabara hiyo ya umeme basi yatarudi katika kutumia mafuta kama kawaida
Ubunifu huu umetoka kwa kampuni ya Siemens ambayo imetoa teknolojia hii kwa magari makubwa kwa kushirikiana na kampuni ya Scania
Ripoti zilizopo ni kwamba zaidi ya theluthi ya hewa chafu (Carbon Dioxide) inatokana na vyombo vya usafiri, hivyo basi teknolojia ni njia moja wapo ya kupunguza machafuko hayo
Ukiachana na Sweden bado kampuni ya Siemens ipo katika plani za kuanzisha eHighway nyingine huko California kwa kushirikiana na kampuni ya Volvo
Majaribio ya teknolojia hii huko Sweden yatafanyika kwa kipindi cha miaka miwili na kama nchi hiyo ikiona ina manufaa kwao basi barabara nyingi za mfumo huu zitatengenezwa
Teknolojia inazidi kukuwa kwa kiasi kikubwa sana na hivi sasa inajaribu kumeza kila kitu. Teknolojia hii ni ya aina yake na pia ni nzuri kwa nchi ambayo ina nishati kubwa ya umeme. Kwa mfano ikija kwa nchi kama Tanzania inaweza ikawa ni tatizo kwani umeme tuu ni shida