WhatsApp ni moja ya programu tumishi ambayo imekuwa ikifanyiwa maboresho mara nyingi tuu ndani ya kipindi kifupi na hii inatokana na ile shughuli ya kufanya watumiaji wake wanaifurahi zaidi lakini tukumbuke mambo yote huanzia kwenye Beta kabla ya kusogezwa kwa wengine.
Mwezi Disemba 2021 WhatsApp waliahidi kufanya maboresho mbalimbali ya programu hiyo tumishi kwa upande wa toleo la majaribio upande Android na iOS kitu ambacho hivi sasa kimeanza kuonekana kwa watu wachache sana ambao wapo kwenye orodha ya “Watu wanaojaribu” maboresho yaliyofanyika kwenye WhatsApp kabla ya wengineo wote.
Kwa mujibu wa WaBetaInfo kupitia WhatsApp Beta toleo namba 2.22.5.4 upande wa Android na wengine wachache wanaotumia WhatsApp ya toleo la majaribio namba 2.22.5.3 wamekiri kuona mabadiliko ya ile sura ya mbele wakati mtu anapoongea na simu. Maboresho mengine ni kuonekana mawimbi ya sauti wakati mtu anapowasiliana na mtu zaidi ya mmoja kwa wakati huohuo.
Kupata majibu kuhusu ombi lako la kuendelea kutumia WhatsApp
Kufungiwa kutumia WhatsApp imeshawatokea watu wengi tuu duniani na hii inatokea iwapo itaonekana mhusika amekiuka makubaliano ya matumizi. Katika kurahisisha vitu pia WhatsApp inafanya maboresho ya watumiaji kuweza kupata majibu iwapo akaunti yake imefunguliwa hivyo kuweza kuwasiliano na watu wake au bado yupo “Kifungoni”.
Maboresho haya (sura mpya) yanaonekana kuwa mazuri ambayo yanalenga kumfanya mtumiaji kuwa mwepesi kutumia WhatsApp kwa ajili ya kufanya mawasiliano.
Vyanzo: Gadgets 360, WaBetaInfo
No Comment! Be the first one.