Baada ya kupatikana kwa muda mrefu katika vifaa vya Apple, gemu la Super Mario linatarajiwa kuachiwa katika vifaa vya Android Machi 23.
Hii itakuwa ni habari njema kwa mashabiki wa gemu hilo ambao wanatumia vifaa vya android, gemu hili limekuwepo katika vifaa ambavyo vinatumia OS za iOS tangu mwezi Desemba mwaka jana.
Je kwanini gemu hili limecheleweshwa kwa watumiaji wa Android?
Watengenezaji wa gemu hili wanasema kwamba walikua wanalifanyia kazi swala la usalama kwa upande wa Android na ndio maana wamechelewa sana kuleta gemu katika OS hii. Shigeru Miyamoto amekiri hayo baada ya katika mahojiano yake na mtandao wa Mashable, katika mahojiano hayo Shigeru amesema wao wamekuwa kila wakati wakijaribu sio tu kutengeneza bidhaa bora bali pia wamekuwa wakipigana kuwapa wateja bidhaa salama.
Kwa mujibu wa tweet kutoka Nintendo America Super Mario itaanza kupatikana kuanzia machi 23 kwa watumiaji wa Android, upo uwezekano mkubwa app hii ikingizwa katika masoko makubwa zaidi kwanza na kisha kufatia masoko madogo kama ya Afrika mashariki.