Dunia ya leo ambayo imejaa utandawazi lukuki inafanya watu wasiwe na ulazima wa kuhifadhi nyimbo/aina nyingine ya burudani kwenye vifaa vyao vya kidijiti na badala yake wawe wanapata huduma hiyo popote pale na wakati wowote ule kiurahisi kabisa.
Takwimu za watu wanaosikiliza muziki mtandaoni duniani kote inazidi kuongezeka mwaka hadi mwaka na hii inatokana na sababu mbalimbali hivyo kufanya makampuni ambayo yanajihusisha na huduma hiyo kuzidi kupata faida kutokana na biashara hiyo.
Kwa mujibu wa takwimu ambazo zimetoka kwa mujibu wa MIDiA zinabainisha kuwa Spotify ndio kinara kwenye huduma watu duani kote kuweza kusikiliza muziki mtandaoni kupitia programu tumishi/tovuti husika. Katika robo ya pili ya mwaka 2021, Spotify iliweza kuwa na 31% ya watuaji wote wanaosikiliza muziki mtandaoni.
Apple Music, ipo kwenye nafasi ya pili kwa kuwa na 15% ya wanaotumia huduma hiyo duniani kote. Nafasi ya tatu imeshikiwa na Amazon Music na Tencent Music kwa wote kuwa na 13% ya wateja wa kusikiliza muziki mtandaoni na YouTube imechukua 8% ya wateja wote ulimwenguni wapatao 523.9 milioni.
Je, Spotify mauzo yake yamepanda/yameshuka kulingannisha na miaka ya nyuma?
Takwimu zinaonyesha kuwa mauzo ya Spotify yameshuka kidogo kulinganisha na miaka miwili nyuma ambapo mwaka 2019 iliweza kukusanya 34% ya wateja wa huduma ya kusikiliza muziki mtandaoni huku mwaka 2020 ilipata 33%.
Kwa takwimu hizo ni wazi kuwa msukumo wa watu kusikiliza muziki mtandaoni bado sio mkubwa na hii inaweza kuwa inachagizwa na mabo kadha wa kadha. Je, mwaka huu ni nani ambaye atashikilia uskani? Spotify wataongoza tena? Endelea kutufuatilia na tutakuhabarisha.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.