SoundCloud ni mtandao au unahusisha muziki wa ‘LiveStream, kuna kuipindi mtandao huu ndio ulikua unaongoza katika nyanja hii
Sifa yake kubwa ilikua ndio kimbilio namba moja kwa watengeneza muziki na wanamuziki kwani walikuwa wana uwezo wa kuweka kazi zao na zikajilikana kiurahisi kupitia mtandao huu.
kama ilivyo katika mitandao mingine na huu pia umeweka wazi rekodi ambazo zimewekwa na wasanii mwaka 2016.
Kwa haraka haraka ni kwamba nyimbo ambayo imeongoza kusikilizwa (stream) ni nyimbo ya Desiigner ijulikanayo kama Panda.
Msanii ambae albamu yake inaongoza kusikilizwa katika mtandao huo ni Albamu ya Chance The Rapper ijulikanayo kama ‘Colouring Book’ katika mtandao wa SoundCloud
2016 ulikua ni mwaka mzuri sana kwa SoundCLoud kwani ndio mwaka ambao kampuni ilijiongeza kwa kiasi kikubwa ili kuhakikisha kuwa inakuwa katika ushindani mkubwa na makampuni mengine ambayo yanajihusisha na huduma ya ‘Live Streaming’
Ndani ya mwaka huo huo kukawa na fununu kuwa mtandao huo upo katika mchakato wa kununuliwa na Spotify (mtandao unaoongoza kwa huduma ya kustream). Licha ya hivyo fununu hizo bado hazijajulikana kama ni za uongo au vipi ingawa asilimia kubwa inabashiri kuwa ni za uwongo.
Taarifa zinasema kwa kiasi kikubwa nyimbo za miondoko ya Hip Hop ndiyo ambayo inaongozwa kusikilizwa katika mtandao huo.
Msanii ambae anongoza kuwa na Followers wengi ndani ya mtandao huo ni Lil Uzi Vert. Japokuwa mtandao huo haukutoa mpagalio wa namba juu ya miondoko ambayo inaongoza kusikilizwa lakini walisema ni miondoko ya hip-hop, pop, electronic, house, na rock.
Miji ambayo inaongoza kutumia mtandao huo wa SoundCloud ni pamoja na London, Los Angeles, Hanoi, Cairo, Berlin, Mexico City, Jakarta, Paris, Chicago, Lima, Toronto, Tokyo, na San Paolo.
Bado nauona mtandao wa SounCloud ukiwa katika jitihada za kuhakikisha kuwa unakuja kutoa ushindani mkubwa kwa mitandao yenye majina makubwa na kwa kufanya hivyo inajikita katika kuhakikisha kuwa inajipatia faida kubwa
Ningependa kusikia kutoka kwako? Je wewe ni mtumiaji mzuri wa mtandao wa SoundCloud? Kama sio niandikie sehemu ya comment hapo chini mtandao ambao huwa unautumia