Hali bado ni tete kwa makampuni mengi ya kiteknolojia, lakini hata hivyo hali ni mbaya kwa kila mtu sio? Snapchat wao wanaona ni bora tuu wapunguze baadhi ya wafanya kazi.
Hii inatokana na kampuni ya Snapchat kuona kwamba kwa kiasi kikubwa sana inakua inapata mapato machache kwa kipindi hichi.
Lakini kwa sasa jambo hili halifanyika bado, kwa sasa inasemekana tuu kuwa kampuni iko na mpango huo wa kupunguza baadhi ya wafanya kazi.
Licha hya hivyo kwa kipindi cha hivi karibuni Snapchat imekua ikijikita Zaidi katika kuhakikisha kuwa ina bidhaa mbali mbali.
Bidhaa kama vile za miwani na hata ile miwani ya AR ni moja kati ya bidhaa kutoka kwao, hata kama unakumbuka zile Drone zao zinazojulikana kama Pixy.
Hii ni kuhakikisha kuwa wanakua na vyanzo mbali mbali vya mapato, lakini bado hali sio nzuri kama vile walivyotegemea.
Kwa sasa kampuni ina wafanyakazi Zaidi ya 6,000 na bado haiko wazi juu ya namba ya wafanyakazi ambao watapumzishwa
Kampuni imepitia mengi sana katika swala la upambanaji ili kuweza kupata mapato, hii imeifanya kampuni mpaka kuanzisha huduma ya mtandao huo ya kulipia, Snapchat Plus.
Kingine ni kwamba kampuni ina kasumba ya kutofanya vizuri katika biashara zake zingine ambazo ziko nje ya mtandao kama vile hizo drone (Pixy) na miwani
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je unahisi kampuni ifanye kitu gani katika kuhakikisha kuwa inapata mapato mazuri bila kupunguza wafanya kazi?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.