Simu za mfumo huu kutoka katika kampuni ya Google zinasubiriwa kwa hamu sana na kwa mwaka huu tulikua tunategemea tupate hata moja kutoka katika kampuni hilo.
Kama unakumbuka kuna hii moja tuliiandika hapa na tulikua tunaitegemea mwisho wa mwaka huu, lakini sasa inatuladhimu tusubiri walau mpaka mwaka 2023.
Kumbuka Google imeshatoa baadhi ya simu zake maarufu zile za Pixel na hata saa janja wameshatoa na kilichokua kikisubiriwa kwa shauku kubwa ikiwa ni hii simu tuu.
Mpaka sasa hakuna sababu ambayo imewekwa wazi kuwa ni kwanini mpaka sasa simu hiyo haijaliona jua, kubmuka simu hii ilikua inabidi itoke tangia mwaka 2011.
Sababu ambayo wameitoa ni kwamba simu haijatoka kwasababu bado uzalishaji/utengenezwaji wake haujakamilika.
Hearing from multiple sources in their supply chain that the Google foldable launch was delayed till next spring… pic.twitter.com/QXr7hhV3ZX
— Ross Young (@DSCCRoss) May 25, 2022
Katika fununu za hapo awali kabisa zilikua zinadai kuwa kampuni imechelewa kuja na kifaa hiki kwa sababu walikua wanafanyia uchunguzi wa miundo (ubunifu) wa aina mbili wa simu hii.
Soma kila kitu kuhusu kujikunja >>HAPA<<
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, hii umeipokeaje? je na wewe ni miongoni mwa wale ambao walikua wanasubiria kwa hamu simu hii.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.