Simu ya Galaxy A11 ni moja ya matoleo toka Samsung ya bei ya chini yenye mwonekano wa kuvutia na thamani nzuri kwa gharama yake.
Kampuni ya Samsung ni kati ya kampuni chache ambazo hutoa matoleo mengi kwa mwaka, yakiwa yamelenga makundi mbalimbali ya wateja.
Sifa za Simu hii ni kama;
- Kioo (Display) cha teknolojia ya TFT chenye ukubwa wa inchi 6.4.
- Mfumo endeshi wa Android 10.
- Qualcomm Snapdragon 450 SoC.
- RAM ya GB 2 au 3, na diski uhifadhi ya GB 32 au 64.
- Mfumo wa kamera 3 (13 MP, 5 MP na 2 MP) nyuma na kamera ya 8 MP mbele.
- Betri yenye uwezo wa 4000mAh
Simu hii inasapoti teknolojia ya mawasiliano ya 4G, lakini pia inasapoti Bluetooth na WiFi kwa kutuma taarifa na kushiriki huduma ya internet. Pia inasapoti huduma ya FM Radio.
Simu hii ina sehem ya kuchomeka earphones na ina sehemu ya kuchomeka waya ya kuchaji simu wa aina ya USB Type-C 2.0. Inaruhusu kuchaji kwa nguvu hadi ya Watt 15 na inapatikana katika rangi nne, Nyeusi (Black), Bluu (Blue), Nyekundu (Red) na Nyeupe (White).
No Comment! Be the first one.