HMD Global ambao tayari wana bidhaa mblaimbali ambazo zinabeba jina la Nokia mwezi huu wa Mei kuzindua simu mbili za Nokia ambazo zilipata kutangazwa mwezi Februari wakati wa onyesho la MWC2019.
Makampuni mengi yanapotaka kuzindua bidhaa mpya mara nyingi huwa wanatoa vidokezo fulani ulani kuhusiana na kitu hicho ambacho wanataka kukileta machoni pa watu. Wakati wa onyesho la MWC2019 HMD Global iliweka wazi kuwa wana Nokia 9 PureView, Nokia 4.2, Nokia 3.2, Nokia 1 Plus na Nokia 201 ambazo watazitoa na tayari baadhi ya simu hizo zimeshazinduliwa.
Noki 3.2 na Nokia 4.2 ni rununu (simu janja) ambazo zinatazamiwa kuzinduliwa Mei 7 huko India na kulingana na kidokezo kutoka kurasa rasmi inaonyesha simu hizo kwenye kitufe cha kuzima/kuwasha simu kitakuwa kinawakawaka iwapo patakuwepo na taarifa fupi. Kwa undani zaidi rununu husika zitakuwa na sifa zifuatazo:-
Kipengele |
Nokia 3.2 |
Nokia 4.2 |
Kioo | Kioo kina urefu wa inchi 6.26 (72081520px) LCD IPS | Kioo kina urefu wa inchi 5.71 (720 x 1520 pixels) |
Muonekamo | Ina umbo la herufi “V” iliyowekwa sehemu ndogo sana kwenye kamera ya mbele | Ina umbo la herufi “V” iliyowekwa sehemu ndogo sana kwenye kamera ya mbele |
Kipuri mama | Qualcomm SDM429 Snapdragon 429 ndio iliyowekwa | Qualcomm SDM439 Snapdragon 439 |
Kipengele |
Nokia 3.2 |
Nokia 4.2 |
Kamera |
Nyuma: Kamera moja-MP 13+LED flash
Mbele: Ina kamera moja yenye MP 5. |
Nyuma: Kamera tmbili-MP 13+MP 2+LED flash.
Mbele: Kamera moja yenye MP 13. |
RAM/Diski uhifadhi |
|
|
Betri |
|
|
Kipengele |
Nokia 3.2 |
Nokia 4.2 |
Bei |
$145|zaidi ya Tsh. 340,700 (32GB) |
$189|zaidi ya Tsh. 434,700 (32GB) |
Rangi |
Nyeusi, rangi ya chuma |
Nyeusi, Udhurungi |
Mengineyo |
|
|
Hizo ndio simu mbili za Nokia ambazo ziazinduliwa ndani ya siku chache zijazo. Vipi wewe msomaji wetu umevutiwa na ipi kati ya hizo mbili?
Vyanzo: Today India, GSMArena