Mpaka sasa dunia nzima inajua kuwa LG itaachana na biashara ya simu janja mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu. Mbali na hilo ni wazi kuwa LG ina wateja wengi sehemu nyingi duniani na ni vyema wakafahamu kuwa simu janja zao zipo kwenye mpango wa kupata masasisho ya Android 11, 12 na 13.
Hivi karibuni LG walitangaza tarehe rasmi ambayo itajiweka pembeni kabisa na biashara ya simu janja lakini wakaweka wazi kuwa watamaliza kabisa rununu walizonazo ndani vilevile kuendelea kutoa masasisho ya programu tumishi kwenye simu zao ingawa itaakuwa ni kwa kipindi fulani tu.
Sasa kwa mujibu wa tovuti za kampuni kwenye nchi za Ujerumani na Korea Kusini wameweka wazi kuwa baadhi ya simu zao zitapokea masasisho ya Android 11, 12 na 13. Hii maana yake ni nini? Hapa wana maana ya kuwa hata mara baada ya kufunga biashara ya simu janja mnamo Julai 31 wateja wenye rununu mbalimbali watapata masasisho ya Android 11, 12 mpaka 13.
Simu ambazo tayari zimeshapokea/zitapokea masasisho masasisho ya Android 11
Tayari kupitia tovuti za LG nchini Ujerumani na Korea Kusini wameshaweka wazi orodha ya rununu ambazo zimeshapokea au zitapata masasisho ya Android 11 kama inavyoonekana pichani.
Vipi kuhusu Android 12 na 13?
Kwenye mpango huo wa LG imeweka wazi kuwa wateja wao pia watapokea masasisho ya Android 12 na 13. Hivyo, wateja wenye simu hizi hamna budi kutabasamu.
LG ndio hao mdogo mdogo wanawaaga wateja wao kwa kutoa habari njema kwao na sisi TeknoKona tumeshaleta mbele yenu taarifa hii. Daima tunasema msiache kutufuatilia.
Vyanzo: Android Authority, Gadgets 360, WCCF Tech
2 Comments