Familia ya simu janja ya Tecno imeendelea kukua baada ya mwanafamilia mpya kuzinduliwa huko Nigeria. Tukiongelea simu janja za Tecno Spark hivi sasa imefikia toleo la 8.
Simu janja za Tecno Spark kwa mwaka huu pekee zimeshazinduliwa takribani 3 ikiwemo na hii ya sasa ambayo imezinduliwa huko Nigeria. Simu hii ipo katika mwonekano wa kisasa lakini unaovutia ambapo betri ya kwenye rununu hii ni kubwa. Sifa nyingine za kuhusu simu hii zinaridhisha kwani zinaendana na menggi ambayo soko la sasa linahitaji. Uchambuzi wake ni kama ifuatavyo:-
Muonekano|Kamera
Tecno Spark 8 ina kioo cha ubora wa IPS LCD chenye urefu wa inchi 6.5 na kama kawaida kamera ya mbele ya MP 8 imepambwa na sehemu iliyoingia ndani kidogo. Kamera kuu ina MP 16, ile ya mbili haijafahamika ni mahususi kwa ajili ya AI+taa ya kuongeza mwanga sehemu hafifu.
Kipuri mama|Uwezo wa betri
Simu hii imewekwa kipuri mama MediaTek Helio P22 amabcho ni chenye nguvu zaidi kulinganisha na kile ambacho kipo kwenye Spark 7 (Helio A25). Kwa upande wa betri lina 5000mAh; inachaji kwa 10W kwa kutumia MicroUSB. Hapa zimepunguzwa 1000mAh kulinganisha na mtangulizi wake halikadhalika haina teknolojia ya kuchaji haraka.
Memori|Mengineyo
Simu janja husika ina RAM GB 2 (GB 3 RAM-Spark 7), diski uhifadhi 64 GB lakini ikiwa na uwezo wa kuweka memori ya ziada. Simu hii inatumia HiOS 7.6, Android 11 Go Edition (tofauti na Android 11). Haitumia USB-C wala teknolojia ya kuchaji bila kutumia waya.
No Comment! Be the first one.