Android 12 ipo karibu kuzindulliwa na kwa muda sasa toleo la majaribio limekuwa likipelekwa kwenye simu janja mbalimbali kama Nokia X20 ili watumiaji hao kupata wasaa wa kutoa maoni yao kuhusiana na toleo la programu endeshi husika.
Watumiaji wa simu janja za Android wengi wao wanafahamu kuhusu toleo la programu endeshi lijalo huku wakiwa na shauku ya kutaka kwenye Android 12. Kwa sasa Android 12 ipo kwenye hatua ya majaribio na hivi karibuni Nokia X20 imewezeshwa halikadhalika watumiaji wake wapo kwenye nafasi ya kutoa maoni kuhusiana na Android 12 Beta.
Je, Android 12 Beta inapatikana kwa yeyote mwenye Nokia X20?
Android 12 Beta kwa wenye Nokia X20 wanaweza kuingia kwenye programu hiyo ya kujaribu toleo hilo la programu endeshi kwenye simu janja zao. Kuna njia mbili za kujisajili:
Mosi, kwa kwenda kwenye kipengele cha “My Phone” kisha kujisajili na baada ya hapo ndani ya 12 utapokea taarifa fupi ya ambapo ndani yake kuna maelekezo ya hatua za kufuata ili kuweza kutumia Android 12 Beta. Kama utataka uweze kujaribu toleo hilo la programu endeshi mapema zaidi basi njia ya pili ni kuingia kwenye Mpangilio (Settings) > About Phone > System Updates dakika 20 baada ya kujisajili.
Ni muhimu kufahamu kuwa toleo la majaribio haliwezi kufanya kazi kwa ufanisi kama Android 12 hivyo inaweza isifanye kazi vyema kwenye simu janja lakini kama utapenda kujaribu Android 12 Beta basi BOFYA HAPA kisha fuata maelekezo.
Vyanzo: GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.