Kwenye ulingo wa simu janja ambazo zina uwezo mkubwa kwa maana ya kuweza kuhimili magemu mazito mojawapo ni Lenovo Legion Y90 ambayo tarehe ambayo rununu hiyo itanzinduliwa imeshafahamika.
Kwa wale wanaopenda rununu ambazo zina uwezo mkubwa hasa kwenye upande wa kuitumia rununu kucheza magemu basi tutakuwa tunafahamu vyema kuwa Lenovo ni miongoni mwa kampuni zinazotengeneza simu za aina hiyo. Simu hii ambayo itatoka Februari 28 ya mwaka huu itatoka huku mtangulizi wake ni Lenovo Legion 2 Pro.
Kuna mengi ambayo bado hayapo wazi kuhusiana na Lenovo Legion Y90 lakini machache kati ya mengi simu hii ina kioo chenye urefu wa inchi 6.92 aina ya AMOLED. Kipuri mama cha kwenye simu janja husika kimeboreshwa na walioitengeneza wameamua kutumia Qualcomm Snapdragon 8 Gen 1.
Simu janja ambazo zinakuwa ni mahususi kwa ajili ya kuzitumia kucheza magemu makubwa uwezo wa betri huwa ni mkubwa tuu unaovutia. Inaaminika kuwa rununu hii inakuja na betri lenye 5600mAh, 68W za teknolojia ya kuchaji haraka huku zikiwa ni betri 2 ndani ya rununu moja kujaa chaji ndani ya dakika 36 tu.
Ujio wa tabiti Lenovo Legion Y700
Siku hiyohiyo ya Februari 28 inaaminika kuwa Lenovo watazindua tabiti yao ambayo pia imetengenzwa kuweza kuhimili magemu mazito-Lenovo Legion Y700 ambapo baadhi ya sifa zake (ingawa si rasmi) ni pamoja na kioo chenye urefu waa inchi 8.8, kamera moja upande wa nyuma, uwezo wa betri-6550mAh na 45W za teknolojia ya kuchaji haraka.
Sasa kazi yetu ni kusubiri bidhaa hizo zitoke tuweze kufahamu undani wake kwa kina lakini pia tujipange mfukoni ili kuweza kuzinunua. Uamuzi tunao sisi wenyewe!
Vyanzo: Gizmochina, GSMArena
No Comment! Be the first one.