Sony Xperia 10 III ni simu janja ambayo kwa sasa inaiweka kwenye ramani kampuni iliyoitengeneza na kwa historia bidhaa zake nyingi zinapata soko linaloridhisha.
Ni miaka mingi sasa tangu simu janja Sony Xperia zitoke (toka Oktoba 27 2008) na hadi leo hii bado zinaendelea kutoka zikiwa zinaboreshwa kulingana na kile kinachohitajika sokoni. Aprili 14 ndio Sony Xperia 10 III ilizinduliwa na sifa zake ni kama ifuatavyo:-
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.0
- Ubora: OLED (1080*2540px); ina uwezo wa kuzuia vumbi/maji kwa kina cha mita 1.5 kwa hadi dakika 30
Memori :
- Diski uhifadhi: 128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada
- RAM: GB 6
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 12, 8 na 8+taa moja ya kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu. Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 4K na 1080px
- Kamera ya Mbele: MP 8+Ina uwezo wa kurekodi picha mnato za ubora wa 1080px
Betri/Chaji :
- Li-Ion 4500 mAh
- USB-C 3.1, OTG, USB Power Delivery+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 30W
Kipuri mama :
- Snapdragon 690 5G
Uzito :
- Gramu 169
Programu Endeshi
- Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi, Bluu, Udhurungi na Nyeupe
- GB 6/128-$521 (zaidi ya Tsh. 1,198,438) bei ya ughaibuni
No Comment! Be the first one.