TCRA kupitia kitengo chao cha ulinzi wa kompyuta wa dharura, TZ-CERT imeleta shindano kwa wanavyuo wachukuao masomo ya teknolojia ambalo litawafanya wanafunzi kuweza kudukua taarifa na kujilinda na mashumbulizi kupitia shindano la kudukua (HACKING COMPETITION).
Shindano hilo lipo kwa ushirikiano na kampuni ya Silensec litawajumuisha wanafunzi wote wa vyuo vya Tanzania watakaojisajili kupitia tovuti yao ya cyberstars. Tanzania inakua nchi ya pili ya Afrika Mashariki baada ya Rwanda kujiunga katika shindano hilo.
picha : cyberstars
Shindano la udukuzi linalenga wanafunzi wa vyuo wenye uri kati ya miaka 18-24 wanaosoma masomo ya Sayansi ingawa hata wale ambao hawasomi masomo hayo lakini wanapenda kufahamu namna ya kulinda taarifa wanaruhusiwa kujiunga kwenye shindano hilo.
Hii ni nafasi kubwa kwa wanafunzi na watu wengine kuonyesha ujuzi wao katika nyanja hii ya udukuzi ambao kwa hili tunaita udukuzi wa faida kiasi kwamba kama utaonyesha uwezo wako mkubwa wa kudukua na kujilinda na mashambulizi basi utakuwa umejiongezea nafasi kubwa ya kutambulika kitaifa na kufikisha ndoto zako kuwa za kweli.