Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari nchini kuhusu wanafunzi wanaohitaji mikopo ya elimu ya juu.
Madai ambayo yamekuwa yakisambazwa mitandaoni ni kwamba mwanafunzi yeyote ambae mzazi wake ana leseni ya biashara hataruhusiwa kupata mkopo kutokana na wazazi wake kuwa na uwezo.
Naibu waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh. William Ole Nasha amesema taarifa hizo si za kweli na amewaomba watanzania kuzipuuza kwani zina lengo la kuichonganisha serikali na wananchi wake.