Wiki hii imekuwa na mambo mbalimbali yayohusu Samsung ambao wamezindua bidhaa zao kadha wa kadha tayari kwa ajili ya sisi watumiaji duniani kote. Rununu ama simu janja Samsung Galaxy M42 5G tayari imeshazinduliwa!.
Samsung ambao wamekuwa wakiendelea kutoa bidhaa mbalimbali za kidijiti wameona inafaa kuleta Galaxy M42 5G ambayo kimsingi inavutia kutokana na kuja na kile ambacho soko inahitaji kwa sasa. Pata kuzifahamu sifa za rununu husika.
Kioo :
- Ukubwa: inchi 6.6
- Ubora: Super AMOLED, ung’avu wa hali ya juu sana+umbo mithili ya tone la maji kwenye kamera ya mbele
Memori :
- Diski uhifadhi: 128GB+uwezo wa kuweka memori ya ziada mpaka TB 1
- RAM: 6GB/GB 8
Kamera :
- Kamera Kuu: MP 48, 8, 5 na 5+taa mbili za kuongeza mwangaza sehemu ambazo kuna mwanga hafifu
- Kamera ya Mbele: MP 20
Betri/Chaji :
- Li-Ion 5000 mAh
- USB-C+uwezo wa kuchaji haraka kwa nguvu ya 15W (saa 36 za kuongea tu au saa 22 za kuperuzi mtandaoni ama saa 34 ukiamua kuitumia kwa kuangalia picha jongefu pekee)
Kipuri mama :
- Snapdragon 750G
Programu Endeshi
- One UI 3.1, Android 11
Rangi/Bei :
- Nyeusi na Kahawia
- GB 6/128-$295 (zaidi ya Tsh. 678,500) na GB 8/128-$322 (zaidi ya Tsh. 740,600) bei ya ughaibuni
Simu hii itaingia sokoni Mei Mosi kwenye masoko mbalimbali ya mtandao kama Amazon, Samsung wenyewe. Sasa ni wewe msomaji wetu kufanya maamuzi yako kujipanga kuinunua au la!
Vyanzo: Gadgets 360, GSMArena
No Comment! Be the first one.