Samsung ni moja kati ya kampuni kubwa kabisa za kutengeneza na kuuza simu licha ya kuwa na uzalishaji mkubwa sana wa simu kwa mwaka, hilo linabadilika mwaka huu.
Unaweza ukawa unajiuliza juu ya sababu inayopelekea hili? ni wazi kuwa kwa mwaka kampuni hiyo inatengeneza matoleo mengi sana ya simu.
Mwaka huu kampuni hiyo ilijikadiria kuwa itasafirisha simu milioni 310 lakini mpaka sasa wanachodai ni kwamba namba hiyo imepunguzwa mpaka simu milioni 280.
Sababu kubwa ya jambo hili ikiwa ni mfumuko wa bei na kwa asilimia kubwa sana umesababishwa na vita ya Ukraine na sababu zingine.
Hapa ni kwamba kampuni itapunguza uzalishaji wake kwa asilimia 35 katika mwezi mei na kisha asilimia 10 katika miezi ijayo.
Lakini hili jambi halijajitokeza kwa kampuni ya Samsung tuu, makampuni mengi tuu kama vile Apple na mengine nayo yakiwa katika mpango wa kuzalisha kidogo zaidi.
Ukaichana na hayo yote hata hivyo uhitaji wa bidhaa nyingi umepungua kwa sasa –hali ni ngumu– jambo ambalo limibadilika kwa kaisi kikubwa.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie katika uwanja wa comment hapo chini.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.